- Musa akawaambia watu, Msiogope, simameni tu, mkauone wokovu wa Bwana atakaowafanyia leo; kwa maana hao Wamisri mliowaona leo hamtawaona tena milele. [Kutoka 14:13]
- Ee Bwana, utete nao wanaoteta nami, Upigane nao wanaopigana nami. [Zaburi 35:1]
- Mwimbieni Bwana wimbo mpya, Kwa maana ametenda mambo ya ajabu. Mkono wa kuume wake mwenyewe, Mkono wake mtakatifu umemtendea wokovu. [Zaburi 98:1]
- Waambieni walio na moyo wa hofu, Jipeni moyo, msiogope; tazama, Mungu wenu atakuja na kisasi, na malipo ya Mungu; atakuja na kuwaokoa ninyi. [Isaya 35:4]
- Bwana ataniokoa na kila neno baya, na kunihifadhi hata nifike ufalme wake wa mbinguni. Utukufu una Yeye milele na milele. Amina. [2 Timotheo 4:18]
- Hata twathubutu kusema, Bwana ndiye anisaidiaye, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini?[Waebrania 13:6]
- atendaye dhambi ni wa Ibilisi; kwa kuwa Ibilisi hutenda dhambi tangu mwanzo. Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa, ili azivunje kazi za Ibilisi. [1Yohana 3:8]
- Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa. [Ufunuo wa Yohana 12:11]
Karibu sana katika blog hii, Na utapata kujifunza mengi kuhusu biblia huku ukishilikiana na ndugu, jamaa na marafiki kujadili maada mbali mbali za biblia. Kama una swali au maoni yoyote juu ya biblia unaweza kutoka comment yako ili upate majibu kutoka kwa jamaa, ndugu na rafiki zako..
Thursday, January 29, 2015
BWANA HUKUPIGANIA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment