- Akasema, Uso wangu utakwenda pamoja nawe, nami nitakupa raha. [Kutoka 33:14]
- Hata walipokuwa wakishuka mwisho wa mji, Samweli akamwambia Sauli, Mwambie mtumishi atangulie, (naye akatangulia), bali wewe simama hapa sasa, ili nikuambie neno la Mungu. [1 Samweli 9:27]
- Naye akawaambia Yuda, Na tuijenge miji hii, na kuizungushia maboma, na minara, na malango, na makomeo; nchi bado ikalipo mbele yetu, kwa kuwa tumemtafuta Bwana, Mungu wetu; naam, tumemtafuta, naye amemstarehesha pande zote. Basi wakajenga, wakafanikiwa. [2 Mambo ya Nyakati 14:7B]
- Mwe na hofu wala msitende dhambi, Tafakarini vitandani mwenu na kutulia. [Zaburi 4:4]
- Umngoje Bwana, uwe hodari, Upige moyo konde, naam, umngoje Bwana. [Zaburi 27:14]
- Ukae kimya mbele za Bwana, Nawe umngojee kwa saburi; Usimkasirikie yeye afanikiwaye katika njia yake, Wala mtu afanyaye hila. [Zaburi 37:7]
- Nalimngoja Bwana kwa saburi, Akaniinamia akakisikia kilio changu. [Zaburi 40:1]
- Acheni, mjue ya kuwa Mimi ni Mungu, Nitakuzwa katika mataifa, nitakuzwa katika nchi. [Zaburi 46:10A]
- Umtwike Bwana mzigo wako naye atakutegemeza, Hatamwacha mwenye haki aondoshwe milele.[Zaburi 55:22]
- Enyi watu, mtumainini sikuzote, Ifunueni mioyo yenu mbele zake; Mungu ndiye kimbilio letu. [Zaburi 62:8]
- Utamlinda yeye ambaye moyo wake umekutegemea Katika amani kamilifu, kwa kuwa anakutumaini.[Isaya 26:3]
- Kwa maana Bwana MUNGU, Mtakatifu wa Israeli, asema hivi, Kwa kurudi na kustarehe mtaokolewa; nguvu zenu zitakuwa katika kutulia na kutumaini; lakini hamkukubali. [Isaya 30:15B]
- Na kazi ya haki itakuwa amani; na mazao ya haki yatakuwa ni utulivu na matumaini daima. [Isaya 32:17]
- bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia. [Isaya 40:31]
- Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea Bwana, Ambaye Bwana ni tumaini lake. [Yeremia 17:7]
- Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho. [Yeremia 29:11]
- Bwana ni mwema kwa hao wamngojeao, Kwa hiyo nafsi imtafutayo. Ni vema mtu autarajie wokovu wa Bwana Na kumngojea kwa utulivu. [Maombolezo 3:25, 26]
- Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu; kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi. [Mathayo 11:28-30]
- Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.[Wafilipi 4:7]
- Kwa sababu hiyo nimepatikana na mateso haya, wala sitahayari; kwa maana namjua yeye niliyemwamini, na kusadiki ya kwamba aweza kukilinda kile nilichokiweka amana kwake hata siku ile.[2 Timotheo 1:12B]
- huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu. [1 Petro 5:7]
Karibu sana katika blog hii, Na utapata kujifunza mengi kuhusu biblia huku ukishilikiana na ndugu, jamaa na marafiki kujadili maada mbali mbali za biblia. Kama una swali au maoni yoyote juu ya biblia unaweza kutoka comment yako ili upate majibu kutoka kwa jamaa, ndugu na rafiki zako..
Thursday, January 29, 2015
KUPUMZIKA KATIKA BWANA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment