- akawaambia hao makadhi, Angalieni myafanyayo; kwa kuwa hammfanyii mwanadamu hukumu, ila Bwana; naye yupo pamoja nanyi katika neno la hukumu. [2 Mambo ya Nyakati 19: 6B]
- Naam, ukiita busara, Na kupaza sauti yako upate ufahamu; Ndipo utakapofahamu kumcha Bwana, Na kupata kumjua Mungu. Kwa kuwa Bwana huwapa watu hekima; Kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu; [Mithali 2:3 , 5, 6]
- Maandalio ya moyo ni ya mwanadamu; Bali jawabu la ulimi hutoka kwa Bwana. [Mithali 16:1]
- Watu wabaya hawaelewi na hukumu; Bali wamtafutao Bwana huelewa na yote. [Mithali 28:5]
- Na roho ya Bwana atakaa juu yake, roho ya hekima na ufahamu, roho ya shauri na uweza, roho ya maarifa na ya kumcha Bwana; na furaha yake itakuwa katika kumcha Bwana; wala hatahukumu kwa kuyafuata ayaonayo kwa macho yake, wala hataonya kwa kuyafuata ayasikiayo kwa masikio yake; [Isaya 11:2 , 3]
- Basi, kwa habari za hao vijana wanne, Mungu aliwapa maarifa na ujuzi katika elimu na hekima; Danieliii naye alikuwa na ufahamu katika maono yote, na ndoto. [Danieli 1:17]
- Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa Mungu, awapaye wote, kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa. [Yakobo 1:5]
- Unifanye kusikia fadhili zako asubuhi, Kwa maana nimekutumaini Wewe. Unijulishe njia nitakayoiendea, Kwa maana nakuinulia nafsi yangu. [Zaburi 143:8]
- Unifundishe kuyatenda mapenzi yako, Kwa maana ndiwe Mungu wangu; Roho yako mwema aniongoze kwenye nchi sawa, Ee Bwana, unihuishe kwa ajili ya jina lako, Kwa haki yako unitoe roho yangu taabuni; [Zaburi 143:10 , 11A]
- mwenye hekima asikie na kuongezewa elimu, na mwenye ufahamu ayafikie mashauri yenye njia.[Mithali 1:5]
- Njia ya mpumbavu imenyoka machoni pake mwenyewe; Bali yeye aliye na hekima husikiliza shauri.[Mithali 12:15B]
- Pasipo mashauri makusudi hubatilika; Bali kwa wingi wa washauri huthibithika. [Mithali 15:22]
- Sikiliza mashauri, ukapokee mafundisho, Upate kuwa na hekima siku zako za mwisho. [Mithali 19:20]
- Kila kusudi huthibitika kwa kushauriana; Na kwa shauri la akili fanya vita. [Mithali 20:18]
- Maana kwa mashauri ya akili utafanya vita; Na kwa wingi wa washauri huja wokovu. [Mithali 24:6]
- Basi msihukumu hukumu ya macho tu, bali ifanyeni hukumu iliyo ya haki. [Yohana 7:24]
- Lakini hekima itokayo juu, kwanza ni safi, tena ni ya amani, ya upole, tayari kusikiliza maneno ya watu, imejaa rehema na matunda mema, haina fitina, haina unafiki. [Yakobo 3:17]
- Kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu kila neno litathibitishwa. [2 Wakorintho 13:1B]
Karibu sana katika blog hii, Na utapata kujifunza mengi kuhusu biblia huku ukishilikiana na ndugu, jamaa na marafiki kujadili maada mbali mbali za biblia. Kama una swali au maoni yoyote juu ya biblia unaweza kutoka comment yako ili upate majibu kutoka kwa jamaa, ndugu na rafiki zako..
Thursday, January 29, 2015
HEKIMA NA MAAMUZI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment