- Nalijilaza nikalala usingizi, nikaamka, Kwa kuwa Bwana ananitegemeza. [Zaburi 3:5]
- Katika amani nitajilaza na kupata usingizi mara, Maana Wewe, Bwana, peke yako, Ndiwe unijaliaye kukaa salama. [Zaburi 4:8]
- Hutaogopa hofu ya usiku, Wala mshale urukao mchana, [Zaburi 91:5]
- Yeye humpa mpenzi wake usingizi. [Zaburi 127:2B]
- Ulalapo hutaona hofu; Naam, utalala na usingizi wako utakuwa mtamu. [Mithali 3:24]
- Usingizi wake kibarua ni mtamu, kwamba amekula kidogo, au kwamba amekula kingi; lakini kushiba kwake tajiri hakumwachi kulala usingizi. [Mhubiri 5:12]
- Yeye huingia katika amani; wao hustarehe katika vitanda vyao, kila mtu aendaye katika unyofu wake.[Isaya 57:2]
- Na ahimidiwe Bwana, aliyewapa watu wake Israeli kustarehe, vile vile kama yote aliyoyaahidi. Halikukosa kupatikana neno lo lote katika ahadi yake njema, aliyoahidi kwa mkono wa Musa, mtumishi wake. [1 Wafalme 8:56A]
- Nawe utakuwa salama, kwa sababu kuna matumaini; Naam, utatafuta-tafuta kando yako, na kupumzika katika salama. [Ayubu 11:18]
- Yeye huingia katika amani; wao hustarehe katika vitanda vyao, kila mtu aendaye katika unyofu wake.[Isaya 57:2]
- Kama ukigeuza mguu wako usihalifu sabato, usifanye anasa yako siku ya utakatifu wangu; ukiita sabato siku ya furaha, na siku takatifu ya Bwana yenye heshima; ukiitukuza, kwa kutokuzifanya njia zako mwenyewe, wala kuyatafuta yakupendezayo, wala kusema maneno yako mwenyewe; ndipo utakapojifurahisha katika Bwana; nami nitakupandisha mahali pa nchi palipoinuka; nitakulisha urithi wa Yakobo baba yako; kwa maana kinywa cha Bwana kimenena hayo. [Isaya 58:13,14A]
- Basi, mlapo, au mnywapo, au mtendapo neno lo lote, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu. [1 Wakorintho 10:31]
- Basi, imesalia raha ya sabato kwa watu wa Mungu. Kwa maana yeye aliyeingia katika raha yake amestarehe mwenyewe katika kazi yake, kama vile Mungu alivyostarehe katika kazi zake. [Waebrania 4: 9 , 10]
Karibu sana katika blog hii, Na utapata kujifunza mengi kuhusu biblia huku ukishilikiana na ndugu, jamaa na marafiki kujadili maada mbali mbali za biblia. Kama una swali au maoni yoyote juu ya biblia unaweza kutoka comment yako ili upate majibu kutoka kwa jamaa, ndugu na rafiki zako..
Thursday, January 29, 2015
KUPUMZIKA NA LIKIZO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment